Pages

Link

Resource

Friday, August 31, 2012

ONA JINSI MASHABIKI WA YANGA WAFURIKA UWANJA WA NDEGE KUMPOKEA MBUYU TWITE






Beki mpya wa Mabingwa wa Kombe la Kagame, Dar Young Africans, Mbuyu Twite akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana akitokea Kigali Rwanda na kupata mapokezi makubwa kutoka kwa mashabiki wa soka.

Mchezaji nyota kutoka timu ya APR ya Rwanda Mbuyi Twite akizungumza na waandishi wa habari kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana, baada ya Yanga kumpa mapokezi makubwa alipowasili jana kukipiga na timu hiyo.

Mbuyu Twite akiwa amevalishwa jezi namba 4 iliyoandikwa Rage

Moja wa mashabiki aliyekuja katika mapokezi ya Mbuyu Twite akiwa amelala chini


Mashabiki wa Yanga.Picha zote na Mdau Francisdande, Habari na Sosthenes Nyoni
---
TWITE, Twite, Twite' kiitikio 'Rage, Rage, Rage' ndiyo wimbo uliotawala jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati beki mpya wa Yanga, Mbuyu Twite alipowasili akitokea Rwanda.

Wimbo huo ulikuwa ukiimbwa na mamia ya mashabiki wa Yanga wake kwa waume waliofurika uwanjani hapo kwa ajili ya kumpokea beki huyo.

Kwa wiki kadhaa Twite aliteka hisia za mashabiki wa timu za Yanga na Simba ambazo ni baada ya beki huyo kusajiliwa na timu hizo kabla ya yeye mwenyewe kuikana Simba na kuamua kuichezea Yanga.

Kitendo hicho, kilisababisha kuzuka kwa malumbano baina ya viongozi wa klabu hizo mbili na kufuatiwa na tamko la Makamu mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange Kaburu kusema kuwa watamkamata Twite na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria atakapokanyaga ardhi ya Tanzania.

Hata hivyo licha ya vitisho hivyo vya Kaburu, hakuna kiongozi yeyote wa Simba aliyeonekana uwanjani hapo kumsubiri beki huyo kwa ajili ya kumtia mikononi kama ilivyotarajiwa.

Mara baada ya kuwasili uwanjani hapo majira ya saa10.30 jioni, Twite alipokewa na viongozi wa Yanga wakiongozwa na katibu mkuu wa timu hiyo, Selestine Mwesigwa na alikabidhiwa jezi namba 4 yenye jina la Rage kama ushindi dhidi ya wapinzani wao Simba.

Mara baada ya kukabidhiwa jezi hiyo, Twite alizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa umati aliouhushuhudia uwanjani hapo ulimpa moyo wa kuona jinsi mashabiki wa Yanga wanavyomjali.

"Nimeshangaa sana kuona watu wengi kiasi hiki, hii inadhihirisha ni kiasi gani mashabiki wananijali, nami nasema sitawaangusha, jambo la muhimu ni ushirikiano tu kutoka kwao na uongozi mzima wa Yanga ili malengo yafikiwe,"alisema Twite.

Alipoulizwa anazungumziaje mpango wa Simba kutaka kumkamata kwa madai ya kuwatapeli, Twite alisema,"kwa sasa siwezi kuzungumzia hilo, nadhani nitafanya hivyo baadaye."

Baada ya mahojiano na Wanahabari, Twite alipanda gari dogo na moja kwa moja msafara ulioongozwa na mabasi yaliyokuwa yamebeba mashabiki wa Yanga ulielekea makao makuu ya klabu hiyo yaliyoko Mtaa wa Jangwani.

0 comments:

Post a Comment

 

Sample text

Sample Text

Sample Text