Pages

Link

Resource

Friday, August 31, 2012

ONA FULL STORY YA KUSAKA VIPAJI MISS ILALA JANA USIKU, SI MCHEZO!



TOP 5 ya vipaji Miss Ilala, kutoka kushoto ni Merry Chizi, Stella Morris, Amina Sangawe, Magdalena Munisi na Mectilda Martin baada ya kutangazwa washindi jana Nyumbani Lounge.






Majaji kazini












Amina Sangawe akirusha kete yake kwa majaji


Wadau wa Urembo kutoka Ukonga nao walikuwepo


Benny Kisaka na Rutta kushoto



Majaji wetu, asante kwa kazi nzuri



Epraim Kibonde na mnazi mwenzake wa Simba, Philipo



Mrembo akionesha kipaji cha kuchora


Kazi ya mapacha ndio hii


Mapacha jukwaani



Ubora wa kazi ni tofauti na umaarufu wa jina...Cheki Mapacha, utafikiri bendi gani sijui la DRC lenye maskani yake Ufaransa



Warembo wakifuatilia shindano hilo, niwarembo wa miaka ya nyuma Ilala na Kinondoni



Mapacha habari nyingine bwana






Mtangazaji mpya wa Times FM 100.5 Gadan G, ukipenda muite Kapteni au Baba Some Food akiwa na asali wake wa moyo...Lady Jidee. upande wangu huku ni Lisa




















VIMWANA watano usiku wa kuamkia leo wamefanikiwa kuingia fainali ya kuwania taji la mrembo mwenye kipaji zaidi katika shindano la Miss Ilala 2012, lililofanyika kwenye ukumbi wa Nyumbani Lounge, Oysterbay, Dar es Salaam.

Vimwana hao ni Merry Chizi, Stella Morris, Amina Sangawe, Magdalena Munisi na Mectilda Martin, ambao waliwapiku wasichana wenzao wengine wanane, Suzan Deodatus, Whitness Michael, na Elizaberth Pertty, Wilmina Mvungi, Zawadi Mwambe, Rehema Said, Diana Simon, Noela Michael na Phillios Lemi.

Mshindi wa taji hilo, atatajwa katika kilele cha shindano la Miss Ilala 2012 kwenye ukumbi huo huo, Septemba 7, mwaka huu.

Shindano hilo lililoanza saa 2;00 usiku, lilipambwa na burudani ya bendi ya mapacha watatu na mastaa kibao wa bongo walikuwepo.

Warembo hao, wamekuwa wakijifua kwa takriban wiki nne sasa chini ya wakufunzi, Slyvia Mashuda ambaye ni Miss Tanzania namba mbili mwaka 2008 na Miss Ilala wa mwaka huo, na Neema Mbuya na Dickson Daudi wa THT katika shoo.

Miss Ilala, yenye rekodi ya kutoa warembo wanne waliotwaa taji la Miss Tanzania kuanzia mwaka 1999, (Hoyce Temu), 2000 (Jacquline Ntuyabaliwe aka K-Lyne), 2002 (Angela Damas Mutalimwa) na Salha Israel anayeshikilia taji hilo kwa sasa, imepania kuendeleza rekodi yake nzuri mwaka huu.

Miss Ilala inahusisha warembo kutoka vitongoji vya Dar City Center, Tabata na Ukonga na inadhaminiwa na Uhuru One, Dodoma Wine, City Sports Lounge, gazeti la Jambo Leo, Nyumbani Lounge, 100.5 Times FM, Redio ya watu 88.4 Cloud's FM na Redds Premmium Cold.

0 comments:

Post a Comment

 

Sample text

Sample Text

Sample Text